Na Mwandishi Wetu, Ufaransa

UBALOZI wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Ufaransa, umekutana na wadau wa Utalii mjini Paris  kwa ajili ya kuonyesha na kufanya uzinduzi rasmi wa filamu ya 'Royal Tour', iliyoigizwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Aidha,  tukio hilo lililofanyika Julai 8,2022 katika ukumbi wa Ubalozi  lilihidhuriwa na  Mhe. Tabia Maulid Mwita ambaye ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar .

Waziri Mwita alikuwa akiiwakilisha Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika katika maadhimisho ya Siku ya Kiswahili Duniani yaliyofanyika Makao Makuu ya UNESCO tarehe 7 Julai 2022.