Mapema Julai, Kampuni ya Simu ya TECNO ilitangaza uzinduzi wa simu yake ya CAMON 19 iliyo na ubunifu wa picha kali za usiku kwa camera yake ya 64MP, bezel nyembamba ya 0.98mm na vipengele vingine vya kuvutia vinavyopendwa na mashabiki.



Muonekano wa TECNO CAMON 19 Pro

TECNO, kampuni ya simu inayotambulika kimataifa sasa imekuwa chapa ya simu mahiri inayoongoza kwa kufanya uzinduzi wa matoleo yake mbalimbali kwa kutumia teknolojia bora kwa watazamaji wake. TECNO pamoja na mawazo yake ya kibunifu na teknolojia ya hali ya juu inatoa mpambano mkali kwa washindani wake.


Sifa kuu za TECNO CAMON 19 Pro 5G

TECNO CAMON 19 PRO Vs INFINIX NOTE 12 VIP

KAMERA

Ikiwa na kamera yake kuu ya 64MP yenye lensi ya glasi ya RGBW iliyotengenezwa kwa ushirikiano na Samsung, kamera ya usiku ya CAMON 19 Pro inaweka viwango vipya vya kunasa kwa usahihi picha angavu katika mazingira ya mwanga hafifu. Hili linakamilishwa kwa kutumia mfumo ambao unaiga mwelekeo wa jicho la mwanadamu na kuruhusu uchakataji wa mwanga wa kipekee, pamoja na lenzi ya kioo ambayo huongeza upokeaji wa mwanga kwa zaidi ya asilimia 208 na kuongeza mwangaza wa picha kwa kiasi kikubwa. Sifa hii imemuacha mbali mpinzani wake Infinix Note 12 VIP yenye camera ya 108MP.


KIOO

TECNO imeendelea na umahiri wake wa kuthibitisha sifa kabambe katika simu zake kwa watumiaji. TECNO CAMON 19 Pro imekuja na bezel nyembamba zaidi yenye inchi 6.8 FHD+, ili kutoa utumiaji wa kina usio na kifani wakati Infinix Note 12 VIP ina kioo chenye 6.7 inches.


MUUNDO

Hata hivyo, TECNO CAMON 19 Pro inajulikana kwa muundo maridadi unaothaminiwa sana. Hapo awali, CAMON 19 pro ilishinda tuzo za IF Design kuwashinda washindani wake wote ikiwemo Infinix Note 12 VIP kwa muundo bora wa bidhaa kwa kuwa na fremu nyembamba sana na muundo mzuri wa kamera tatu za pete mbili na mipako inayofanana na almasi milioni 200 unaosaidia kuepuka uchafu wa alama za vidole. Hii ni tuzo ya kwanza ya TECNO katika shindano la kimataifa la ubunifu, na kuthibitisha kujitolea kwa kampuni hiyo katika uvumbuzi wa kiteknolojia na mafanikio endelevu.




BEI ya kununua

TECNO CAMON 19 Pro inauzwa kwa bei rafiki zaidi ya Tsh 660,000ikilinganishwa na Infinix Note 12 VIP ambayo inauzwa Tsh 820,000.




TECNO CAMON 19 Pro

Bei na Upatikanaji wa TECNO CAMON 19 Series

TECNO CAMON 19limekuja katika matoleo matatu ya CAMON 19, CAMON 19 Pro na CAMON 19 Pro 5G ambayo itawasili mwishoni mwa mwezi Julai. Bei ni Tsh 450,000 kwa CAMON 19 (128+4GB), Tsh 510,000 kwa CAMON 19 (128+6GB), Tsh 660,000 kwa CAMON 19 Pro, na Tsh 790,000 kwa CAMON 19 Pro 5G. Tembelea duka lolote la TECNO au duka la Vodacom ili kujipatia simu hii.

Agiza mtandaoni kupitia INALIPA;https://www.inalipa.co.tz/stores/tecno#/

Kwa maelezo zaidi piga namba;0744 545 254 or 0678 035 208.