Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA), imepiga marufuku vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kutoonyesha wimbo wa ‘Mtasubiri’ ulioimbwa na msanii Diamond Platnumz akimshirikisha Zuchu.
 
Video hiyo iliyotoka mwezi mmoja uliopita mpaka sasa imeshatazamwa zaidi ya mara milioni kumi kwenye mtandao wa Youtube na ni moja kati ya nyimbo zilizoko katika EP yake First of All (FOA) ukiwa wimbo namba nne.