Wizara ya Ulinzi ya Urusi inasema makombora yake yameharibu ghala kubwa la silaha za jeshi la Ukraine huko Kryvyi Rih - mji alikozaliwa Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky.

Msemaji wa wizara hiyo Igor Konashenkov anadai katika muda wa saa 24 zilizopita zaidi ya wanajeshi 300 wa Ukraine wameuawa.

Pia anadai kuwa ngome kadhaa za kijeshi yameshambuliwa, ikiwa ni pamoja na mfumo wa ulizi wa Urusi kudungua ndege ya kivita ya Ukraine chapa SU-25 mjini Dnipro.

Anasema: "Kwa jumla, kutokana na mashambulio ya angani, zaidi ya wanajeshi 300 na hadi vitengo 50 vya kijeshi na silaha za wanajeshi wa Ukraine ziliharibiwa."