JESHI la Kujenga Taifa (JKT) limewaita vijna waliohitimu elimu ya Sekondari kidato cha sita kwa mwaka 2022 kutoka shule zote za sekondari Tanzania Bara kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kuanzia tarehe 3 Juni 2022 na mwisho wa kuripoti ni tarehe 17 Juni 2022.

Akitoa taarifa kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Kujenga Taifa Mkuu wa Tawi la Utawala wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema sanjari na wito huo Jeshi la Kujenga Taifa JKT limewapangia makambi watakyokwenda kuripoti na mwisho wa kuripoti ni Juni 17, 2022.

==>>BOFYA HAPA KUTAZAMA MAJINA