Wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wamempitisha Mbunge wa Ilala, Mussa Azzan Zungu kuwa mgombea wa nafasi ya Naibu Spika wa Bunge, jijini Dodoma,  Jumanne Februari 8, 2022.

Zungu amepitishwa na wabunge wote wa CCM baada ya Kamati Kuu ya chama hicho kupitisha jina lake pekee kati ya wabunge 11 wa chama hicho waliokuwa wakiomba kuteuliwa kugombea nafasi hiyo.