Takriban wanajeshi 70 wameuawa katika shambulio la mizinga la Urusi, maafisa wa Ukraine wamethibitisha.

Wafanyakazi wa dharura wanajaribu kutafuta manusura katika Kituo cha kikanda cha Kherson ambacho sasa kimezingirwa na wanajeshi wa Urusi, zinasema ripoti, huku wanajeshi na vifaa vya kijeshi vimeripotiwa kuwepo "pande zote".

Jeshi la Urusi linaendelea kusonga mbele kwa kasi huko Kyiv, na picha za satelaiti zinazoonyesha msafara wa kivita ambao una urefu wa maili 40 (65km.

Makumi ya raia waliuawa mapema Jumatatu katika shambulio la makombora la Urusi kwenye mji wa pili kwa ukubwa nchini Ukraine, Kharkiv.