Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya Wizara ya Afya,   Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Wizara ya Ardhi, Nyumba na   Maendeleo ya Makazi, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Ofisi ya Wakili Mkuu wa   Serikali, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Wakala wa Usalama na Afya  Mahali pa Kazi (OSHA) na Halmashauri ya Wilaya ya Ulanga, anapenda kuwataarifu  Waombaji Kazi wote walioomba kazi katika taasisi tajwa hapo juu kuwa usaili unatarajiwa  kuendeshwa kuanzia tarehe 04 – 06 Desemba, 2021 na hatimaye kuwapangia vituo vya  kazi waombaji kazi watakaofaulu usaili huo.
 

Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:-
i. Usaili utafanyika kuanzia tarehe 04 – 06 Desemba, 2021 kama ilivyooneshwa  kwenye tangazo hili; muda na sehemu ambapo usaili utafanyika umeainishwa  kwa kila Kada;
ii. Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa  Barakoa (Mask);
iii. Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi;

==> Kuona Majina ya Walioitwa kwenye Usaili, BOFYA HAPA