Je ni kweli baada ya Infinix Zero X pro sasa kampuni ya simu za mkononi Infinix kuja na simu ya kwanza kwenye toleo la NOTE kuwa na ukubwa mara mbili zaidi ya matoleo ya awali ya NOTE?
 

Hivi punde picha yenye muonekano wa simu ikiwa imeandikwa ‘THE NEXT NOTE PLAY BIG’ imeonekana kuvuja kwenye mitandao ya blog za tech lakini pia kwenye kurasa ya @infinixmobile Infinix imetupia picha inayoashiria ujio wa simu mpya kupitia post inayosema ‘FIRST 11, ARE YOU READ FOR THE FIRST ROUND? Kushabihiana kwa hizi sentensi mbili mashabiki wametafisiri kuwa huenda hii ni simu mpya aina ya NOTE 11.
 

 Simu za toleo la Infinix NOTE hukubalika zaidi kutokana na muonekana mzima wa simu hizi ambao ni imara na wenye kuvutia lakini kivutio kikubwa zaidi kwa simu hizi ni ubora wake wa camera zenye teknolojia ya AI. 

Kamera za simu za toleo la NOTE huimarishwa kwa kila toleo jipya kama ilivyokuwa kwa NOTE 8 ikiwa na camera yenye MP48 na NOTE 10 ikiwa na MP64.

 Tetesi zinadai kuwa simu hii huenda ikaja na kioo cha aina ya AMOLED na hii ni baada ya kampuni hiyo kuonyesha kuwa inawezekana kutumia teknolojia ya hali ya juu na bado simu ikiwa na bei rafiki kama ambavyo tumeliona hili kwa Zero x pro.
 

Je ni sifa gani nyengine ya kipekee kuja katika simu hii  https://bit.ly/3BHedZw?...

Tembelea;  https://www.infinixmobility.com/smartphone/note-11-pro/ kupata majibu kamili ya simu hii mpya ya Infinix NOTE 11.