Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi,imetupilia mbali pingamizi lililowasilishwa na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu la kutaka kesi inayowakabili isisikilizwe na mahakama hiyo kwakuwa haina mamlaka ya kusikiliza kesi zenye mashtaka ya ugaidi.

Uamuzi huo umetolewa leo, Septemba Mosi, 2020 na Jaji Elinaza Luvanda ambaye baada ya kupitia hoja za pande zote mbili amesema Mahakama yake ina mamlaka ya kusikiliza mashauri ya ugaidi na kwamba pingamizi lililowasilishwa na upande wa utetezi halina mashiko na hakubaliani nalo.