Askofu Josephat Gwajima ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kawe na Jerry Silaa wa Jimbo la Ukonga mkoani Dar es Salaam kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ambao ni wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge wameondolewa kwenye kamati hiyo.

Uamuzi huo umetolewa leo Agosti 24, 2021 hadi itakapoamuliwa vinginevyo Bungeni jijini Dodoma.

Askofu Josephat Gwajima na Jerry Silaa wameitwa mbele ya kamati hiyo wakituhumiwa kusema uongo, kushusha hadhi na heshima ya Bunge.

Kamati hiyo ina jumla ya wajumbe 24 wakiwamo Gwajima na Silaa na sasa imebaki na wajumbe 22 baada ya hatua hiyo.