Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA), jana  limetangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha sita na ualimu uliofanyika mwezi Mei mwaka huu.

Akitangaza matokeo hayo jijini Zanzibar, Katibu Mtendaji wa NECTA Dkt. Charles Msonde amezitaja shule kumi za Sekondari zilizofanya vizuri katika mtihani huo ambazo ni ;

1. Kisimiri (Arusha)

2. Kemebos (Kagera)

3. Dareda (Manyara)

4. Tabora Girls (Tabora)

5. Tabora Boys (Tabora)

6. Feza Boys (DSM)

7. Mwandet (Arusha)

8. Zakia Meghji (Geita)

9. Kilosa (Morogoro)

10. Mzumbe (Morogoro)