Serikali imeanza safari ya utoaji tuzo mbalimbali kwa wadau wa sekta za Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo zitakazoenzi vipaji na mafanikio katika sekta hizo.

Hayo yameelezwa jana usiku wa Julai 3, 2021, katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere, Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo aliyemwakilisha Waziri wa Wizara hiyo Mhe Innocent Bashungwa.

Dkt. Abbasi alikuwa akitoa nasaha katika usiku wa tuzo mbalimbali kwa wanafunzi wa vyuo vikuu katika sanaa mbalimbali, tuzo zilizoandaliwa na taasisi ya UniAwards kwa kushirikiana na Wizara ya Habari na Sanaa.

“Tuzo za leo ambazo tumeshirikiana na wadau wa sekta binafsi ni mwanzo wa mwaka huu kuwa wa kurejesha tuzo nyingine mbalimbali ambazo zitaenzi na kutambua umahiri katika sekta zote nne za wizara yetu,” alisema.

Tuzo hizo zimehudhuriwa na mastaa mbalimbali wa muziki na filamu wakiwemo Kala Jeremire, Baker Flavour, Jay Melody, Rapture na Lissa wake, Davina, Batuli, Joti na wengine wengi.