Kesi ya unyang’anyi kwa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai Lengai ole Sabaya pamoja na wenzake wawili,imeahirishwa mara baada ya shahid wa upande wa jamhuri kupata dharura.

Wakili wa serikali kwenye kesi hiyo Trasila Gervas ameiambia mahakama mbele ya hakimu wa mahakama ya hakimu mkazi Salome Mshasha kuwa shahidi waliyempanga ameshindwa kufika mahakamani hapo nakuahidi mashahidi kuwepo mahakamani july 16,2021