Rais Samia Suluhu Hassan amemuapisha Kampeni Mstaafu George Mkuchika kuwa Waziri katika Ofisi ya Rais Ikulu, Kazi Maalum.

Kabla ya kuteuliwa kushika wadhifa huo, Kampteni Mstaafu Mkuchika alikuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, nafasi inayoshikiliwa hivi sasa na Mohamed Mchengerwa.

Hafla ya kuapishwa kwa Kapteni Mstaafu Mkuchika imefanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma, ambapo pia Makatibu Tawala wa mikoa walioteuliwa hivi karibuni na Rais Samia Suluhu Hassan wameapishwa.