Rais Yoweri Museveni amekula kiapo hii leo nchini Uganda kuliongoza taifa hilo kwa muhula wa sita.


Museveni ataiongoza Uganda kwa miaka mengine mitano, ikiwa ni muhula wake wa sita madarakani.

Aliingia madarakani Januari 1986 kwa mapinduzi ya kijeshi, hadi utakapofika uchaguzi mwingine 2026 atakuwa madarakani kwa miaka 40, sawa na miongo minne. Wakati huo akiwa na umri wa miaka 81.

Alishinda uchaguzi wa Januari 14, 2021 kwa kuwabwaga wagombea wengine kumi katika nafasi ya Urais kwa ushindi wa asilimia 58 ya kura zote.