Sio wengine tena ni wale wale nguli wa simu za Mkononi Tanzania wanakuja na mazawadi kibao kwa wale watakao nunua simu mpya ya Infinix HOT 10T. 

Katika uzinduzi wa Promotion ya nunua na ushinde zawadi iliyotambulishwa na Meneja Mauzo wa Infinix Bi. Winifrida Chumi alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Sports Arena kinachoruka kupitia Kituo cha redio ya Wasafi FM alitangaza zawadi zitakazotolewa ni Jiko la Gesi, jiko la Umeme pamoja na Air coolers kama zawadi kubwa.


Pia zawadi ndogondogo ni pamoja na Vikombe, Headphones, Wireless Keybords na zingine kibao. Promotion hii ni kuanzia Tarehe 6/5 mpaka Tarehe 25/5 katika maduka yote ya simu.

Unaweza kujiuliza ni nini cha ajabu kwenye hii simu? Akielezea sifa za simu hii mpya Bi. Eddah Charles ambae ni Afisa Elimu na Mafunzo wa kampuni ya Infinix amesema simu hii kwanza kabisa ina kamera bora yenye uwezo wa mp48 inayokuwezesha kupata picha zenye rangi halisia ya eneo husika vile vile ina wigo mpaka wa kioo cha ukubwa wa nchi6.82” ambacho ni HD+ (Kioo ng’aavu), na processor G70 yenye speed ya ajabu na kuifanya simu yako kuwa nyepesi wakati wa utumiaji.


Sifa nyengine ambayo ni ya ziada Infinix HOT 10 T PEEK PROOF inakifanya kioo cha simu yako kuwa cheusi na kumnyima uwezo wa kuona aliyepo pemebni yako hivyo kutohitaji kuweka glass protector ya Privacy.

Aisee jiunge na wajanja wenzako mjini kwa kujipatia simu yako ya HOT 10T ukatambe na wanao kitaa. Kwa mengi Zaidi tembelea www.infinixmobility.com
au piga nambari ya simu 0744606222.