Kwa mara ya kwanza series ya HOT kutoka kampuni ya simu Infinix kubeba sifa ya toleo la Infinix NOTE na Infinix S. Tulishazoea kuona toleo la HOT likitamba na nguvu ya battery Safari hii inasemekana kukawa na tofauti kubwa kwenye simu iyo inayodhaniwa kuwa ni Infinix HOT 10T.

Si kama vile tulivyozoea inasemekana Infinix HOT 10T kuja na camera kali yenye MP48 na Mediatek Helio G70 processor na pasipo kusahau ujazo wa battery unaosadikika kuwa mAh 5000 au zaidi.

Vijana wengi hasa wanafunzi wameonyesha matarajio mengi na kuamini kupitia HOT 10T basi wataepuka kero ya simu kupata moto wakati wa uchezaji games lakini pia watahifadhi kazi za kujisomea kwa wingi pasipo simu kugoma goma (stuck).
 

Inasemekana simu hii kuzinduliwa kesho majira ya saa 1:00 ambapo tukio zima litakuwa mubashara kupitia @infinixmobiletz. Uzinduzi huu utashareheshwa na japo la wasanii kutoka kwenye Sanaa ya music ambao ni Billnass anaekimbiza na wimbo wa ‘TATIZO’na Frida amani anaekimbiza na wimbo wa Madame President pamoja na wengine wengi.


Tembelea https://www.infinixmobility.com/ kujua mengi kuhusu bidhaa za Infinix.