Wasanii watatu wa Afrika wameteuliwa kuwania tuzo za BET nchini Marekani.Wasanii hao ni Diamond Platinumz , Wizkid na Burnaboy kutoka Nigeria pamoja na wasanii wa Ufaransa .

Burnaboy aliibuka mshindi wa orodha hiyo mwaka uliopita . Wasanii hao watawania tuzo ya mwanamuziki bora wa kimataifa.

Tuzo za BET zitafanyika tarehe 27 mwezi Juni na watu watahudhuria tamasha lake baada ya kufanyika kwa video mwaka uliopita kwasababu ya mlipuko wa virusi vya corona.