Dar es Salaam, 6/5/2021-Kampuni ya simu TECNO inayotamba kwa uzalishaji wa simu wa viwango vya hali ya juu na kwa bei rafiki kuzindua rasmi TECNO Camon 17pro simu ya kwanza kwa tolea la TECNO CAMON kuja na Selfie Camera ya MP48 na teknolojia ya 4K video resolution kwa kushirikiana na Tigo, Atsoko, DSTV na Coca Cola. 


TECNO Camon 17pro imekuwa ni gumzo kupitia mitandao ya kijamii kwa muda na kila mtu akionyesha shahuku ya kumiliki kifaa hicho kipya kutoka TECNO. Kampuni ya simu TECNO kupitia mtandao wa kijamii @tecnomobiletanzania imeweka wazi TECNO Camon 17pro kuzinduliwa 7/5/2021 ikiambatana na ofa mbalimbali kutoka kwa washirika wake. 


TECNO Camon 17pro, simu inayosemekana uwekezaji wake mkubwa upo kwenye Camera kuja kuwa suluhisho kwa Videographers na Photographer katika shughuli zao za upigaji picha na uchukuaji video. Camera ya nyuma ya Camon 17pro ni MP64 ambayo ni bora zaidi wakati wa kuchukua filamu kwa kutumia white and black mode.  


Kampuni ya simu TECNO imekuwa ikiwalenga zaidi vijana kupitia mtiririko wa matoleo mbalimbali kama vile Spark, Pop, Phantom, Pouvoir na Camon zote kubeba applications ambazo ni pendwa kwa vijana. 


Kufahamu mengi zaidi kuhusu bidhaa za TECNO tembelea www.tecno-mobile.com