Maelfu ya Watu nchini Marekani, wanaendelea kushangilia hukumu ya kwanza, iliyomtia hatiani Polisi wa Kizungu kwa mauaji ya Mtu mweusi (George Floyd), katika historia ya Taifa hilo.
Hata hivyo, Rais wa Marekani Joe Biden amesema kutiwa hatiani kwa Derek Chauvin, kwa mauaji ya George Floyd, kunaweza kuwa hatua kubwa, katika vita dhidi ya ubaguzi wa kimfumo, lakini hakutoshi.
Viongozi hao wawili wamelitolea wito Baraza la Congress, kuyashughulikia haraka mageuzi ya Polisi, ikiwemo kuidhinisha muswaada wa sheria uliopewa jina la Floyd, aliyeuawa akiwa amegandamizwa goti shingoni, mwezi Mei mwaka jana.