Marekani imelaani shambulio la waasi wa Houthi nchini Yemen dhidi ya vituo vya mafuta vya Saudia Arabia na kusema waasi hao hawaoneshi kujitolea katika juhudi za amani zinazoongozwa na nchi hiyo. 

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani Ned Price amesema kuwa kundi la waasi wa Houthi nchini Yemen lazima lioneshe kujitolea kwake kushiriki katika mchakato wa kisiasa wa kuafikia amani nchini humo baada ya kundi hilo kudai kuhusika katika mashambulio ya ndege zisizo na rubani na makombora dhidi ya Saudi Arabia.