Na mwandishi wetu

Marais wastaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, viongozi waandamizi wa Serikali na mabalozi waonaziwakilisha nchi zao hapa Nchini wamewataka watanzania kuendelea kudumisha uzalendo, fikra na maono aliyokuwa nayo Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ili kuiwezesha Tanzania kukua kimaendeleo

Akizungumza mara baada ya kusaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Kikwete amesema kifo cha Hayati Magufuli hakikutarajiwa hasa wakati huu ambapo taifa lilimuhitaji na kuwasihi watanzania kudumisha mema aliyoyaasisi kwa maslahi ya taifa.

“Kwa kweli kifo chake hakikutarajiwa, tulitegemea kwa kweli aendelee kuliongoza taifa kwani katika mhula wake wa kwanza aliliongoza taifa vizuri sana…….naamini kuwa yale ambayo hayakukamilika, Rais wa Jamhuri ya Tanzania mhe. Samia Suluhu Hassan atayaendeleza kikamilifu,” Amesema Dkt. Kikwete na kuwasihi watanzania kuendelea kudumisha uzalendo, fikra na maono aliyokuwa nayo Hayati Dkt. Magufuli.

Rais wa Awamu ya Pili, Mhe. Alhaji Ali Hassan Mwinyi nae amefika katika viwanja vya Karimjee na kusaini kitabu cha maombolezo akifuatiwa na Aliyekuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mohamed Gahib Bilali, Jaji Mkuu wa Tanzania Mhe. Prof. Ibrahim Juma na pamoja na Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Biswalo Mganga.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai nae pia amefika na kusaini kitabu hicho akifuatiwa na Spika wa Baraza la Wawakilishi la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar mhe. Zubeir Ali Maulid ambaye amesema kuwa Hayati Magufuli katika kipindi kifupi cha uongozi wake amefanya mambo mengi yatakayosalia kuwa historia katika taifa la Tanzania.

“Msiba huu ni wetu sote watanzania na umetugusa sana kwani  hayati Magufuli ameyafanya mengi katika mhula wake wa kwanza ambapo mengi hayo tumekuwa tukinufaika nayo sisi watanzania…..kwa sasa tushikamane kudumisha umoja wetu ili kuweza kusonga mbele kimaendeleo,” Amesema Mhe. Maulid

Aidha, mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini nao wameungana na watanzania kuomboleza kifo cha Hayati Dkt. Magufuli kwa kusaini kitabu cha maombolezo ambapo baadhi yao wamemuelezea kuwa katika uhai wake Hayati Magufuli alitamani kuiona Tanzania inayojitegemea kiuchumi na watu wake kuondokana na umasikini.

Naibu Balozi wa Burundi nchini Tanzania, Mhe. Prefere Ndayishimiye amesema kuwa msiba wa Hayati Magufuli umewagusa sana kwani alikuwa kiongozi aliyependwa na kujulikana na bara lote la Afrika.

“Amefanya maendeleo makubwa ambapo naamini kuwa vizazi vijavyo vitayaona na kuendeleza pale alipoishia Dkt. Magufuli,” Amesema Naibu Balozi

Kadhalika, mbali na viongozi wastaafu pamoja na viongozi waandamizi wa Serikali wananchi wa kada mbalimbali wamejitokeza kwa wingi kusaini kitabu cha maombolezo na kumuelezea hayati Magufuli kuwa alikuwa kiongozi aliyeweka maslahi ya nchi mbele kwa manufaa ya watanzania.

Rais wa Mstaafu wa awamu ya pili Mhe. Alhaj Ali Hassan Mwinyi akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi 2021 

Rais wa Mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kilichotokea tarehe 17 Machi 2021 


Makamu wa Rais, Mstaafu Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 


Jaji Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati John Pombe Joseph Magufuli  


<

Spika wa Baraza la Wawakilishi la Serikali ya Mapinduzi Zanzibar mhe. Zubeir Ali Maulid akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli   


Balozi wa Oman nchini Tanzania, Mhe. Ali Abdulla – Al Mahrouq akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  


Balozi wa Somalia nchini Tanzania, Mhe. Mohamed Hassan Abdi akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  


Balozi wa Misri nchini Tanzania, Mhe. Mohamed Gaber Abulwafa akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  


Balozi wa Sudan nchini Tanzania, Mhe. Jaafer Nasir Abdalla akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli   


Naibu Balozi wa Italia nchini, Mhe. Roberte Cocconi akisaini kitabu cha maombolezo katika viwanja vya Karimjee kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli