Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limemthibitisha Dr. Philip Mpango kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa 100%.

 Wabunge waliopiga kura ni 363 na wote wamepiga kura ya NDIO, hakuna kura iliyoharibika.

Rais Samia Suluhu Hassan alimpendekeza Philip Mpango kuwa makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Jina hilo liliwasilishwa bungeni asubuhi ya leo Jumanne na mpambe wa Rais katika bahasha maalum.