Staa wa muziki wa Rap kutoka Nchini marekani Bobby Shmurda ameachiliwa kutoka gerezani Februari 23, 2021.

Rapa wa Kundi la Migos Quavo tayari ameenda kumchukua Rapa huyo kwa ndege yake binafsi kama alivyoahidi.


Siku ya leo itakuwa ya furaha zaidi kwa Mama wa Bobby Shmurda Leslie Pollard ambaye amekuwa akiisubiri tarehe ya leo kwa hamu sana, Leslie siku jana aliiambia TMZ kuwa mara Bobby atakapoachiliwa kutoka gerezani kutakuwa na hafla ndogo kufurahia chakula cha jioni na familia yake.

Rapa huyo Mzaliwa wa Miami alifungwa jela tangu mwaka 2014 akishtakiwa kwa makosa mbalimbali ikiwemo kula njama ya kufanya mauaji, Biashara za dawa za kulevya na umiliki wa Silaha kinyume cha sheria.