Na Mwandishi wetu,
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge ameonesha kutoridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa majengo ya mihadhara katika chuo cha Diplomasia na kumuagiza Mkandarasi anayetekeleza mradi huo kuzingatia thamani ya fedha, muda wa mkataba na ubora.

Balozi Ibuge ametoa maagizo kwa Mkandarasi huyo ambaye ni Kampuni ya Casco Construction pamoja na mshauri muelekezi Ask architects wakati alipotembelea mradi huo katika chuo cha Diplomasia leo jijini Dar es Salaam kusema kuwa endapo Mkandarasi hata fanya hivyo atakuwa amekiuka masharti ya mkataba na mkataba wake utasitishwa mara moja.

“Huu mradi ni mradi wenye maslahi ya Taifa majadiliano yaishe leo mkataba ulishaisha tangu mwezi Disemba 2020, hizi ni hela za walipa kodi…..nataka nione thamani halisi ya fedha [Value for Money] ya walipa kodi katika mradi huu, siatakubali kupoteza fedha za walipa kodi,” Amesema Balozi Ibuge

Katibu Mkuu ameuagizo pia uongozi wa chuo hicho kuhakikisha kuwa unasimamia ujenzi wa majengo hayo kwa karibu zaidi na umakini ili kuiwezesha serikali kupata thamani halisi ya fedha katika mradi huo wenye maslahi mapana ya Taifa.

Awalia akiongea na wahadhiri pamoja na wafanyakazi katika chuo hicho Balozi Ibuge amewataka wote kwa pamoja kuhakikisha kuwa wanatekeleza diplomasia ya uchumi kutokana na mabadiliko ya dunia.

“Najua mmeanzisha mitaala inayogusia masuala ya diplomasia ya uchumi hadi mmeanza kuanzia baadhi ya matawi katika baadhi ya mikoa hili ni jambo jema, lakini uwezo wa nyinyi kuleta [link] ya utekelezaji wa diplomasia ya uchumi ambao ndiyo Wizara yetu inasimamia…unapohusisha na nchi nyingine ni lazima utafiti wenu pamoja na kuboresha wigo wa utekelezaji wa diplomasia ya uchumi,”

Balozi Ibuge ameongeza kuwa diplomasia ya uchumia inaambatana na siasa pamoja na diplomasia ya utamaduni wetu hasa kwenye lugha ya kiswahili hiyo ndiyo sehemu ya mahusiano yetu na wengine.

“Urathi wa ukombozi kusini mwa Afrika anayehusika ni Tanzania sasa Chuo cha Diplomasia ambapo ndipo mawazo mazuri ya namna bora ya sisi kuhakikisha tunaiendeleza na kuishindania na kuhakikisha hakuna mwingine wa kushindana na sisi, njia pekee ni kupitia kwenu nyinyi na tafiti zenu,” Amesema Balozi Ibuge

Kwa upande wake Mkandarasi anayetekeleza mradi huo Mhandisi Cosmas Salufu kutoka kamupuni ya ujenzi ya Casco, pamoja na mshauri elekezi mhandisi Ally Simbano kutoka kampuni Ask Architects kwa pamoja wameahidi kutekeleza maagizo ya Katibu Mkuu na kuhakikisha kuwa thanami halisi ya fedha inapatikana katika mradi huo.