Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, 76, amepiga kura ikiwa zimesalia chini ya dakika 15 kabla ya vituo vya kupiga kura kufungwa.



Vituo vya kupiga kura vimefungwa saa kumi jioni ingawa watu waliokuwa kwenye foleni wanaruhusiwa bado kupiga kura.

Rais Museveni, amekuwa madarakani tangu mwaka 1986, na sasa anawania muhula wa sita.

Mpinzani wake mkuu akiwa Bobi Wine,38, mwanamuziki aliyeamua kuwa mwanasiasa.

Rais amepiga kura katika mji wa Rushere Magharibi mwa nchini Uganda.