MABINGWA wa kihistoria Nchini timu ya Yanga imejiwekea rikodi nzuri katika

mashindano ya Mapinduzi kwa kutoruhusu kufungwa bao hata moja hadi sasa wakai

mashindano yanayoendelea  katika hatua ya Nusu fainali.

Katika Michezo 2 iliyocheza Yanga walitoka sare ya 0-0 mbele ya Jamhuri

kisha kuwafunga bao 1-0 Namungo, ambapo ndio timu pekee msimu huu katika

Mashindano hayo kumaliza dakika 180 (michezo 2) pasipo kuruhusu lango lake kuguswa.

Hata hivyo Yanga kwa msimu wa 15 wa Mashindano ya Mapinduzi imeweka rikodi ya kuwa

timu ya kwanza kujihakikishia kutinga hatua ya Nusu fainali baada ya kumaliza

michezo miwili na kuwa na alama Nne na kuongoza kundi A,lenye Timu ya Namungo na

Jamuhuri ya Pemba.

Mashindano hayo yaloshirikisha timu 9 mwaka huu timu zote 8 zimeruhusu

lango lao bao isipokuwa Yanga pekee.

Hatua ya nusu Fainali ya Mashindano ya Kombe la Mapinduzi yamechezwa LEO  katika

Dimba hilo la Amani ambapo Yanga dhidi ya Azam saa 10: 15 jioni huu Wekundu

wa Msibazi Simba dhidi ya Namungo saa mbili na robo usiku.

zitachezwa