Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (Wakwanza kushoto) akimkabidhi Cheti cha Kutambua Ujasiri na Utendaji Kazi Askari wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Koplo Denis Minja, aliyeokoa maisha ya mtoto wa miaka miwili aliyekuwa ametumbukia kwenye shimo la choo Mjini Karagwe. Tukio hilo limefanyika leo katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo Mtumba, Jijini Dodoma.