Kampuni ya simu Infinix Mobile LTD inasema tukae mkao wa kula. Je ni nini tutegemee kutoka Infinix?


Na kama ni simu mpya je nisimu kutoka series gani na kama ni valentine campaign basi watujuze tuanze kujichanga mapema ...nimewazatu.


Nikiwa bado najiuliza ni nini hasa Infinix kutuletea mapema mwaka huu? lakini pia tufahamu Infinix imekuwa kampuni imara na iliweza kuthibitisha hilo mwaka jana ambapo COVID-19 iliweza kusimamisha biashara nyingi lakini kwa Infinix bado walisimama imara nakuendelea kutupa simu zilizo bora kama vile Infinix NOTE 8 inayoendelea kutamba sokoni kutokana na ubora wake wa MP16 za camera ya mbele na MP64 za camera ya nyuma.


Uimara wa kampuni hii kunazidi kunipasha shauku ya kutaka kujua ni nini kipo njiani,lakini kwa taarifa zilizopo chini ya pazia ni kwamba Infinix itakuja na moja ya simu kabambe na huenda ikawa tishio kwa simu zote zenye kupatikana sokoni kwa bei isiyozidi sh. 350,000 huku baadhi ya sifa zikitajwa kupitia tovuti mbalimbali kwa kuusifu zaidi uwezo wa battery yenye mAh6000 kudumu na chaji kwa muda mrefu pamoja na ubora wa resolution yenye kukifanya kioo cha HOT 10 play kioo6.82 HD kuwa ang’avu wakati wote. 


Tembelea https://www.infinixmobility.com/tz/ ili kufahamu mengi zaidi.