Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imevunja rekodi kwa kukusanya mapato ya Shilingi Trilioni 2.088 ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 101, katika robo ya pili ya mwaka wa fedha wa 2020/2021 ikilinganishwa na Shilingi Trilioni 1.664 iliyokusanywa katika robo ya kwanza iliyoishia mwezi Septemba mwaka 2020.

Akitoa taarifa hiyo jijini Dar es salaam, Kamishna Mkuu wa TRA Dkt Edwin Mhede amesema, kiwango hicho cha ukusanyaji.mapato kimevuka lengo walilojiwekea la kukusanya Shilingi Trilioni 2.072.

Amewaambia Waandishi wa habari kuwa, ongezèko hilo la ukusanya mapato kwa kiasi kikubwa limechangiwa na mwamko wa Walipa kodi ambao wamekuwa wakilipa kodi zao kwa hiari.

Kwa mujibu wa Dkt Mhede, Idara ya walipa kodi wakubwa  kwa  mwezi Desemba mwaka 2020 pekee ilikusanya takribani Shilingi Trilioni Moja, Idara ya forodha ilikusanya mapato ya asilimia 97 ikikuatiwa na Idara ya walipa kodi.