Hatua ya nusu Fainali ya Mashindano ya Kombe la Mapinduzi zitachezwa

leo Jumatatu katika Uwanja wa Amaan kati ya Azam FC vs Yanga Sc

Saa 10:15 jioni na Simba Sc vs Namungo FC saa 2:15 Usiku .

Hayo ni Mashindano ya 15 tangu yalipoanzishwa rasmi mwaka 2007 ambapo

 Simba Sc na Mtibwa Sugar zinaongoza kucheza fainali nyingi zikicheza

mara 6 kila timu.

Simba ambayo imecheza fainali 6, tatu ikitwaa Ubingwa na 3 ikipoteza

 (2008,2011,2015,2017,2019 na 2020).

Mtibwa Sugar nayo imecheza fainali nyingi (6) za Mashindano hayo ambapo

 wameshinda 2 na kupoteza 4 (2007, 2008, 2010, 2015, 2016 na 2020).

Azam ikishika nafasi ya tatu kucheza fainali nyingi za Mashindano hayo

ambapo imecheza fainali 5 na zote imetwaa Ubingwa (2012, 2013, 2017, 2018 na 2019.

Yanga wamecheza fainali 2 wakishinda 1 na kupoteza 1 (2007 na 2011)

sawa sawa na URA ya Uganda ikicheza fainali 2 wakishinda 1 na wakipoteza 1 (2016 na 2018).