Raia wa Uganda hii leo wanapiga kura kumchagua rais na wawakilishi wapya wa bunge .

Akizungumza siku ya Jumatano mwenyekiti wa tume ya uchaguzi nchini humo jaji Simon Byabakama aliserma kwamba wapiga kura wa kiume ni zaidi ya milioni tisa huku wenzao wa jiniai ya kike wakiwa zaidi ya milioni tisa.

Katika uchaguzi huo rais Yoweri Museveni ambaye anatetea wadhfa wake anakabilia na upinzani mkali kutoka kwa mwanamuziki wa zamani maarufu Bobi Wine.

Bobi Wine ni mgombea ambaye amevutia iddai kubwa ya vijana nchini humo. hatahhivyo rais Museveni anajivunia utawala wake wa muda mrefu ambapo amefanya baadhi ya maenedeleo.

Robert Kyagulanyi, maarufu Bobi Wine, anasema kuwa anawakilisha kizazi kipya cha vijana wa nchini humo, huku Yoweri Museveni, 76, akisema kuwa anasimamia ustawi.