Mange Kimambi Ameandika Haya:

"Najua mlikuwa mnasubiria tamko la dada wa taifa aisee kwa mara ya kwanza dada enu sina la kusema maana issue imenichanginyi *in Bambo’s voice * 🤣


Kusema kweli mimi mwenyewe sio mara ya kwanza kusikia hii habari, yani katika ubuyu niliwahi kuletewa mara nyingi nikapuuzia huu ni namba 1, yani ilikuwa nasoma sentensi ya kwanza alafu nasonya kinigeria nasema kimoyomoyo ‘ huyu chizi nini, eti yule sio babake, eti Ricardo kakake’ yani hakuna watu nilikuwa nawaona mabogus kama waliokuwa wananiletea hii habari 🤣


Anyways, issue iko hivi, hii story sio siri kwa wanafamilia na wenyewe walipanga kuimwaga kwenye reality show yao ili watengeneze pesa, walikuwa wanasubiria reality show ndo waimwage ila Esma ndo akaunguza picha juzi alivyosema Mke wa Ricardo alitembea na Msizwa. Ikabidi Ricardo na mkewe wajiteteee kuwa mkewe na Esma wanachuki za kiwifi na si mengineyo. Isingekuwa Esma kuharisha juzi wala wasingeongelea mpaka wafanye reality show.


Nasikia Dai ana mdogo wake wamefanana kindakindaki, walitaka kuja kumtoa kwenye reality show.


SHINDA ZAWADI YA SIMU KWA KUDOWNLOAD APPP YA Tujuzaneblog HAPA


Naskia Esma ugomvi wake na huyo Malaika ni wivu wa Dai, naskia Dai anampenda sana huyo shemeji yake kutwa anamsifia mzuri, na kuna sherehe hapo nyuma Dai aliingia na huyo Malaika ukumbini, unaambiwa Esma alinuna balaa.Malaika alipofungua duka Esma akadhani Dai ndo kamfungulia akampigia simu Malaika akamwambia naona mpaka Dai kakufungulia duka sasa wewe ni shemeji au shemeji kula? 🤣🤣.Yani unaambiwa Esma bifu na Malaika ni Diamond anavyompenda huyo shemeji yake, Malaika hakutaka tu kumuingiza Dai kwenye hiyo story. Esma wivu anaamini Malaika anatembea na Dai. Na kuna siku Dai aliposti duka la huyo malaika, Esma kidogo afe mnaambiwa.Hii story sina wasiwasi nayo, bifu lao ni Dai sio Msizwa. Esma akaona amuharibie kwenye familia kwa kusema anatembea na Msizwa.

Esma bwana anamuita Ricardo zoba sasa kuna mwanaume Zoba zaidi ya Petit 🤣. Mitusi yote ile Petit karudi na wanaishi wote Sinza kwenye nyumba aliyopanga Msizwa 🤣.

Kwenye hii issue mwenye makosa yote ni Bi Sandra, angemueleza kwanza Mzee Abduli kabla ya jamii" Mange