Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Hudson Kamoga amemsimamisha kazi Ofisa Mtendaji wa kijiji cha Haydom, Adela Kente kwa madai ya kupigana hadharani kinyume na sheria ya Utumishi wa Umma.
Amesema amemuandikia barua ya kumsimamisha kazi na pia ameunda kamati ya kuchunguza suala hilo ili kutoa maamuzi mara baada ya uchunguzi wa tukio hilo kufanyika

“Mtumishi kupigana ni utovu wa nidhamu ameidhalilisha ofisi ya mkurugenzi ambaye ni mwajiri wake tulichokifanya tumemsimamisha kazi,” Kamoga.