BAADA ya dakika 90 kukamilika sasa ni matuta yataamua nani atakuwa bingwa wa Kombe la Mapinduzi 

Simba wanaanza kupiga penalti ya kwanza  Uwanja wa Amaan, timu zote zinaomba dua kwa sasa

Shikalo na Beno Kakolanya wanatakiana kila la kheri

Shikalo anakaa langoni na Kahata anakwenda kupiga penalti ya kwanza

Kahata anafunga kwa mguu wa kushoto, Shikalo anafungwa.

Beno anakaa langoni na Tuisila anafunga bao la Kwanza kwa Yanga mguu wa kulia

Shikalo anakaa langoni Kagere anagongesha mwamba.

Beno anakaa langoni Ninja anafunga.


Shikalo anakaa langoni, Mugalu anafunga

Beno anakaa langoni Tonombe anapiga shuti Beno anaokoa

Shikalo anakaa lango Onyango anapiga Shikalo anaokoa
Beno langoni Mauya anafunga
Shikalo langoni Gadiel anafunga

Ntibanzokiza anafunga penalti ya 4 kwa Yanga.

Yanga 4-3 Simba

Bingwa wa Kombe la Mapinduzi ni Yanga