Nyota wa muziki nchini, msanii Damond Platnumz amevunja rekodi ya kufikisha YouTube views Million 1 ndani ya muda mfupi zaidi kupitia video ya wimbo wake mpya "Waah" aliyomshirikisha Koffi Olomide.

Awali rekodi hiyo ilikua inashikiliwa na Mwanamuziki Davido Kutoka nchini Nigeria.

Diamond ameweka rekodi hiyo mpya baada ya kufikisha views Milion 1 ndani ya Masaa 8 TU. Kwa upande wa Davido yeye alifikisha views Milion 1 ndani ya Masaa 9 pekee kupitia Video ya wimbo wake FEM.