Tanzania na Indonesia zimeahidi kushirikiana na kuendeleza kukuza biashara kwa kuanzisha kwa manufaa ya nchi zote mbili.  

Akihutubia katika usiku wa shukrani kwa ajili ya wafanyabiashara wa Tanzania na Indonesia kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kukuza biashara na uwekezaji kati ya nchi hizo mbili, Balozi wa Indonesia nchini Tanzania Mhe. Prof. Ratlan Pardede amesema kuwa maendeleo yaliyopatika kwenye sekta ya biashara nzuri inayofanywa na wafanyabiashara kutoka nchi zote mbili.

"Sisi Indonesia na Tanzania tumekuwa tukifanya biashara yenye manufaa kwa mataifa yetu mawili, bidhaa tunazouza ni imara na zimekuwa na ubora mzuri ambapo kwa sasa biashara imeongeza mapato zaidi ya asilimia 10," Amesema Balozi Pardede  

Ameongeza kuwa mwaka 2017 aliahidi kuwaleta wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Indonesia kuja Tanzania kwa ajili ya kuwekeza, ambapo hadi sasa tayari wameanzisha kiwanda cha Sabuni na Losheni Mkuranga

Kwa upande wake Mgeni Rasmi, ambaye ni Waziri wa Biashara na Uwekezaji kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Mudrik Ramadhan Soraga amempongeza Balozi kwa hatua na mipango mizuri ya kuinua uchumi wa mataifa yote mawili na kumuahidi ushirikiano katika kuhakikisha kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kuwaboreshea mazingira wawekezaji na wafanyabiashara ili kuwawezesha kufanya biashara vizuri katika mazingira salama.

Nataka nikuhakikishie kuwa Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya biashara kati ya Indonesia na Tanzania kwa kiwango cha juu." Amesema Soraga. Pia Mhe. Waziri alielekeza wakati mwingine Baraza la kuundwe Biashara la Tanzania na Indonesia (TIBC) ili mpango huo uweze kujumuisha zaidi na kuwafikia wadau wengi nchini Tanzania.

Kulingana na rekodi za Ubalozi wa Indonesia, bidhaa takribani 54 za Kiindonesia zipo kwenye soko la Tanzania kama vile mafuta ya Mawese, nguo, karatasi pamoja na sabuni. Kwa upande mwingine, Indonesia imekuwa ikiagiza bidhaa kadhaa kutoka Tanzania, ambazo ni karanga, pamba, kakao, kahawa, chai, viungo na tumbaku.