WAKATI watu wakiwa bize na habari ya P Funk na binti yake Paula, mara paap staa wa filamu Bongo Elizabeth Michael ‘Lulu’ naye akakiamsha baada yamkujibu kejeli shabiki yake mtandaoni ambaye alikuwa anajaribu kumpa ushauri juu ya uchumba wake na Majizzo.“

 

Lulu unaweza mfungulia kesi Majizzo kwa kuchelewesha ndoa, mbona sheria hiyo ipo, we hujasikia yule dada wa Ndola Zambia kamfungulia kesi mchumba wake, mwaka unaisha huu hakuna ndoa anakupigisha viuno kihuni tu,” Aliandika Paul Michael“

 

Huyo dada wa Zambia itakuwa aliingia uchumba bila riba, mimi uchumba wangu una riba, yaani ndoa inavyochelewa muda mrefu dau (deni) ndo linazidi.“ Mnaweza kunisaidia kuacha kiherehere? Mnaniharibia ugali wangu (tusi kubwa),” Lulu alimjibu shabiki huyo.