Lava Lava Amefunguka Haya Makubwa Kuhusu yeye" Nilitamani Kuacha Muziki Meja Kunta Akaniokoa"

Leo Naomba Niwape Story Kwakifupi Juu Ya Hii Project Ya Wimbo Wa #wanga : Mwanzoni Wa Huu Mwaka Wa 2020 Kwaupande Wangu Haukuwa Mzuri Sana Yani Kunamazingira Nilikuwa Napitia kibinadamu Mpaka nikahisi Sio Kawaida Najua Wengi Watakuwa Wamenielewa Nini Namaanisha Kiufupi Nilikuwa Namawazo Sana Mpaka kufikia Wakati Nilitamani kabisa Niache Hata mziki Wenyewe Ndipo Nilikutana Na Mdogo Wangu @mejakunta_ Kwamara Yakwanza Nakutana Nae Pia Alikuwa Anamawazo Sana Kuhusu Ile Skendo Yake Ya Kifo Alichanganyikiwa Kiukweli Nae Hakujua Aanzie Wapi Nawala Hajui Ilo Swala Lilikuwa Vipi Na Ataeleza Nini Kwawananchi Ingali Bado Mzima Katika Maongezi Maongezi Yetu Tukawaza Kwanini Sisi kama Wasanii Tusifanye Kitu ambacho kitawasilisha Hisia Zetu Kwamuda Ule Au Mawazo Yetu Basi Tukaamua kwenda Studio Muda Ule Ule ila kabla Hatuwenda Studio Swali Likaja Tunaanzia Wapi Au Tunafanya wimbo Wa aina Gani Mana kama unavyojua @mejakunta_ Nimuimbaji Wa Singeli Namimi sijawahi kuimba Singeli Ila Niliamini Hakuna kitu kitashindikana Japo Meja alikuwa Anawasiwasi Sana Nauongozi wake Labda pengine Sitoweza Huwezi Amini niliwambia Uongozi Wa Meja Kua Nimepata Aidia Ya Wanga yani /wachawi kutokana Namazingira Tunayopitia itafaa Sana Nakwahapa Nitoe Pongezi Kwama Angu Mzazi kiukweli Nilimpgia Simu nikamuuliza Nataka kuimba singeli Nasijawahi Kuimba Nina Aidia Ya wanga Nifanyaje Akaniambia Kuna Sound Za nyimbo flani zakizamani Kama zile segere Zile Yani Yale Ma VANGA Tumieni Nahisi Itafaa Sana kwamnachotaka Kufanya Kweli Akanitumia link Tofaut tofauti Tukapata Moja Tukaingia Studio Kitu Ambacho Wengi Hawakijui Nikwamba Wimbo Wa Wanga kwanza Nihisia Zakweli kabisa chapili Tulirekodi Siku Moja Tu Ukamalizika Kila kitu Nakesho Yake Ukatoka Hapa Naomba Management Yangu itanisamehe Mana Hakuna Hata Mmoja Aliekuwa Anajua Yani Sikutoa Taarifa kwakiongozi Yoyote Hata diamond 💎 Walishtukia Tu Wimbo Uko YouTube kitu Nilichojifunza Hapa Kwanza Tusikate Tamaa hata kama unapitia Magumu kiasi gani (PAMBANA) Chapili kitu Ukikipenda Naukakifanya Toka Moyoni Watu Watakipenda Tu Muziki Naupenda Na Naimani kuna Siku Nitafika Ninapopataka Mungu Yupo #mwendapolehajikwai #wakatiwamungunisahihikulikowamwanadamu