Usiku wa kuamkia leo Jumatatu 21-12-2020 lilifanyika tukio kubwa la utoaji tuzo nchini Marekani, ambapo  Kumetolewa tuzo za #aeausa2020 ambapo katika tuzo hizo Wasanii watatu wa muziki wa Bongo Fleva kutoka Tanzania yaani Diamond Platnumz, Rayvanny na Nandy wamefanikiwa kushinda tuzo hizo kwenye vipengele tofauti tofauti.

Mbali na Diamond Rayvanny na Nandy kushinda tuzo pia DJ Sinyorita kutoka Clouds Fm amefanikiwa kushinda tuzo ya DJ bora.

Diamond ametangazwa mshindi tuzo za @aeausa 2020 katika kipengele cha “Best Male Artist” (Msanii Bora wa Kiume) akiwashinda Eddy Kenzo, Wiz Kid , Shatta Wale, Stonebwoy, Davido, Burna Boy, Mohamed Abbas, Fally Ipupa na Jahllano ambao alikuwa akichuana nao kwenye Kipengele hicho.

Huku Rayvanny akitangazwa mshindi tuzo za @aeausa 2020 katika kipengele cha Best Male Artist – East/South and North Africa akiwashinda Elgrande toto, The Ben, Diamond Platnumz, Alikiba

Eddy Kenzo, Harmonize, Tewodros kassahun AKA Teddy Afro, Jah Prayzah na Bruce Melodie.


Kwa upande wa Nandy ametangazwa mshindi tuzo za @aeausa 2020 katika kipengele cha “Best Female Artist” akiwashinda Zahara, Yemi Alade, Tiwa Savage, Sho Madjozi

,Sha Sha, Sheebah Karungi, Rema Namakula, Aya Nakamura na Kenza Morsli .


DJ pekee kutoka Tanzania DJ Sinyorita ameshinda kipengelea cha DJ bora akiwashinda DJ Moh

2. DJ Cuppy

3. DJ Slick Stuart & DJ Roja

4. DJ Shimza

5. DJ Nelasta

6. DJ Tunez

7. DJ Xclusive

8. DJ K Meta

9. DJ Roma


Hii hapa chini ni orodha ya washindi wote wa tuzo hizo.


1. Best Male Artist: Diamond platinumz

2. Best Female Artist: Nandy

3. Best Hip Hop/Rap Artist: Elgrande Toto

4. Hottest Group: Sauti Sol

5. Best Collaboration: Beyonce ft Shatta Wale – King Already

6. Best Music Video: Burnaboy – Anybody

7. Entertainer of the Year: Eddy Kenzo

8. Best Dancer/Group: Fire K Stars

9. Best DJ: DJ Sinyorita

10. Best Francophone Artist: Soul Bangs

11. Best Palop Male Artist: Mr Bow

12. Best Palop Female Artist: Yasmine

13. Best New Artist: Laycon

14. Song of the Year: Master KG – Jerusalema

15. Best Upcoming/Local Artist: KG

16. Best Male Artist – Central/ West Africa: Stonebwoy

17. Best Male Artist – East/South/North Africa: Rayvanny

18. Best Female Artist- Central/ West Africa: Yemi Alade

19. Best Female Artist – East/South/North Africa: Zahara

20. Best African Comedian: Eric Omondi

21. Best Gospel Artist: Sinach

22. Best Blogger/ Influencer: The Hot Jem

23. Best Dance Hall Artist: Winky D

24. Best Host TV/ Radio: Douglas Lwanga