Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP), Biswalo Mganga ametoa ufafanuzi kuhusu kumfutia mashitaka kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Nusrat Hanje ambaye alivuliwa uanachama Novemba 27 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habari, Biswalo amesema kesi ameifuta yeye kwa mamlaka aliyonayo kisheria chini ya kifungu cha 91 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai.

Amesema wanaolalamika kuwa amemfutia kesi kada huyo kinyume na taratibu wanakiuka utaratibu .

Biswalo amesema sheria ipo na inafanyakazi zake na hakuna kufanya kazi kwa upendeleo.