Bendera ya Marekani ilibuniwa mwaka 1958 na Robert Heft wakati huo akiwa Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 17, aliibuni kama sehemu ya project ambayo Mwalimu aliwapa na alipomaliza Mwalimu mwanzoni alimpa B- .


Kwakuwa kulikuwa na mpango wa kumpelekea Bendera Rais ili achague inayofaa kuwa ya Taifa, Robert alimuhakikihia Mwalimu kuwa yake itachaguliwa na Mwalimu ataona aibu na kumpa A+, kama alivyotabiri kati ya Bendera tofauti 1500 alizopewa Rais Dwight Eisenhower aliichagua ya Robert na Mwalimu akabadili alama na kumpa A+ .


Robert alizaliwa January 19,1941, na alifariki December 12, 2009 kwa maradhi ya moyo akiwa na miaka 68, hii ni baada ya kuugua pia Kisukari kwa muda mrefu, licha ya kubuni Bendera ya Marekani yenye nyota 50 (zinazowakilisha idadi ya Majimbo USA) , alibuni pia yenye nyota 51 ili itumike pale Jimbo jingine likiamua kujiunga na USA.