Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema katia Nafasi yake ya Uwaziri kwa Awamu hii ya Pili ataanza kushughulika na Bei ya Saruji iliyopanda kiasi cha kulalamikiwa


Katika hotuba yake baada ya kuapishwa amesema, amewapa Wakuu wa Mikoa ambao pia walihudhuria hafla hiyo muda hadi Novemba 20 saa nne asubuhi wawe wamekwenda kwenye Viwanda na kwa Mawakala wa Saruji kujua kwa nini bei imepanda


Amesema, upandaji wa Bei ya Saruji hauna sababu ya msingi kwa kuwa Serikali haijaongeza Kodi na Miundombinu ipo, na waliohitaji Gesi waliwapelekea, pia Makaa ya Mawe yapo mengi