Wabunge 19 wa Viti Maalum Chadema leo Jumanne Novemba 24, 2020 wameapishwa na Spika wa Bunge,  Job Ndugai katika viwanja wa Bunge mjini Dodoma.


Ndugai alikuwa na mkutano leo bungeni lakini kabla ya kuanza kwa mkutano huo, walionekana baadhi ya wabunge hao ambao baadhi walikuwa wabunge katika Bunge lililopita.


Baadhi ya walioapishwa ni Halima Mdee, Grace Tendega, Esther Matiko, Jesca Kishoa na Ester Bulaya.