Chama tawala nchini Ivory Coast kimewaonya viongozi wa upinzani dhidi ya jaribio lolote la kusababisha vurugu nchini humo baada ya kukataa matokeo ya uchaguzi wa Jumamosi ambapo Rais aliye madarakani Alassane Ouattara aliwania kuchaguliwa tena kwa muhula wa tatu.
Upinzani ambao ulisusia uchaguzi huo umeitisha maandamano kuzuia kile wanachokielezea kama uchaguzi wa kulazimisha madaraka.
Bwana Ouattara ameanza kuchukua uongozi wa mapema kwa kupata asilimia 99 ya kura katika baadhi ya maeneo ambayo ni ngome ya chama tawala.
Zaidi ya watu 30 wameuawa katika ghasia za Bwana Ouattara alitangaza kwamba anagombea tena baada ya aliyekuwa amechaguliwa na chama chake kumrithi kufariki dunia ghafla mwezi Julai.
The post Upinzani Ivory Coast waonywa dhidi ya vurugu baada ya matokeo ya uchaguzi appeared first on Bongo5.com.