
Katika Utabiri wao, TMA imesema mvua zinatarajiwa kunyesha katikati mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro,Tanga, visiwa vya Mafia, Unguja na Pemba.
Zinatarajiwa kuanza leo hadi Novemba 10, 2020 na kwamba inatarajiwa maeneo hayo yatakuwa yenye tahadhali kubwa hususani leo na kesho ambapo vipindi vikubwa vya mvua vinatarajiwa kujitokeza
Aidha TMA wamesema, athari mbali mbali zinaweza kujitokeza ikiwa ni pamoja na mafuriko kwenye makazi ya watu, baadhi ya barabara kufungwa na shughuli za kiuchumi kusimama.