Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Joseph Nyamhanga ,ametangaza ajira za walimu wa shule za msingi na Sekondari zipatazo 13,000 huku akiwataka wote walioweza kupata ajira hizo kuripoti ndani ya muda uliopangwa.
Akitangaza mbele ya waandishi wa habari jijini Dodoma Mhandisi Nyamhanga amesema kuwa walimu hao wanapaswa kuripoti ndani ya siku 14 kuanzia Desemba Mosi hadi 14 na wale ambao watashindwa kuripoti ndani ya muda huo nafasi zao zitachukuliwa na walimu wengine.
 





MAJINA YA WALIMU WOTE WALIOPANGIWA SHULE ==> TAZAMA HAPA