Kuanzia Singapore hadi mji wa New York, zaidi ya asilimia 26 ya mabilionea 2,095 duniani wanaishi katika miji kumi ya mabara matatu.
Kati ya mabilionea 2,095 wa mwaka 2020 katika orodha ya mabilionea duniani, 552 wanaishi katika miji 10 pekee.
Na kwa mwaka wa sita mfululizo, mabilionea wengi zaidi wanaishi mji wa New York City.
HONG KONG: Una mabilionea 71
Umepoteza mabilionea 8
Utajiri ukiwa eneo hilo ukiwa ni: dola bilionea 321
Tajiri Mkuu zaidi hapa ni LEE SHAU KEE, mwenye dola bilioni 28.1
Mji wa Hong Kong pia umekuwa mji wa pili wenye mabilionea wengi duniani huku mji mkuu wa Korea Kusini ukapoteza matajiri 10.

MOSCOW: Mabilionea 70
Umepoteza bilionea 1
Utajiri wa eneo ni: Dola bilioni 301.7
Bilionea tajiri zaidi ni: Vladimir Potanin, akiwa na dola bilionea 19.7

Moscow ni miongoni mwa miji 10 yenye mabilionea wa dunia.
Mbali na Shenzhen, ambapo kila bilionea utajiri wake yaani sio wa kurithi, wengi wana ushirikiano wa karibu na rais wa Urusi Vladimir Putin.
Kwa jumla utajiri wa mabilionea wa mji huo ni dola bilioni 424, ikiwa umeshuka kwa dola bilioni 45.7 ikilinganishwa na mwaka mmoja uliopita.
BEIJING: Bilionea 67
Umeongeza mabilionea 6
Jumla ya mabilionea: Dola bilioni 218.2
Tajiri mkubwa eneo hilo ni Zhang Yiming, dola bilioni 16.2

China imedumisha sifa yake kama nchi yenye miji mingi zaidi iliyoingia kwenye kundi la miji 10 yenye mabilionea wengi duniani huku mji wa Shanghai na Beijing ikishika namba 6 na 4 mtawalia.
Mji wa Kusini mashariki mwa Asia ulipata mabilionea 9 wapya tangu mwaka 2019.
Kupanda kwa gharama ya maisha na ushindani wa kimataifa tayari kulikuwa kumeathiri idadi ya matajiri kabla hata ya kuingia kwa virusi vya corona ambako kumefanya mabilionea 23 kuondolewa kwenye orodha hiyo.
NEW YORK: Bilionea 92
Umeongeza mabilionea 8 tangu 2019.
Kulingana na jarida la Forbes, mwaka huu mabilionea 92 wanaishi katika mji wa New York ikiwa imeongeza mabilionea wanane zaidi ikilinganishwa na mwaka mmoja uliopita.
Mwanzilishi wa kampuni ya Bloomberg LP na aliyekuwa Meya Michael Bloomberg, aliyetumia zaidi ya dola billion 1 kati ya utajiri wake wa dola bilioni 48 katika kampeni ya urais iliyoshindwa kabla ya kujiondoa kwenye kinyang’anyiro hicho cha kuingia Ikulu mnamo mwezi Machi na kumzindua Joe Biden.
Mabilionea wengine wakazi wa mji wa New York ni pamoja na nyota wa muziki mtindo wa hip-hop Jay-Z na Julia Koch na mjane wa aliyekuwa mkuu wa kampuni ya Koch David Koch.
LONDON: Bilionea 6
Imeongeza bilionea mmoja.
Utajiri wa eneo: Dola bilioni 212.7
Tajiri mkubwa duniani: LEN BLAVATNIK, Dola bilioni 17

SHANGHAI: Bilionea 46
Imeongeza bilionea 1
Jumla ya utajiri: dola bilioni 130.7
Mkazi tajiri zaidi ni: Colin Huang, akiwa na utajiri wa dola bilioni16.5
SHENZHEN: Bilionea 44 billionaires
Mji huu umeongeza mabilionea 5
Jumla ya utajiri: dola bilioni 220.2
Mkaazi tajiri duniani ni Ma Huateng, mwenyekiti na Mkuu wa kampuni ya Internet media behemoth Tencent Holdings, ni wa pili kwa utajiri nchini China, baada ya mwanzilishi wa kampuni ya Alibaba, Jack Ma.
MUMBAI: Bilionea ni 38
Imeongeza bilionea 1
Mkaazi tajiri ni: Mukesh Ambani, kwa dola bilioni 36.8
Mumbai iliongeza bilionea 1 tangu 2019, umepoteza watano na kuongeza wengine 6 wapya
SAN FRANCISCO: Bilionea 37
Umepoteza mabilionea 5
Mkazi tajiri zaidi eneo hilo ni : DUSTIN MOSKOVITZ, dola bilionea 9.3
SINGAPORE : Mabilionea 31
Imeongeza mabilionea 9
Singapore iliingia kwenye orodha ya kundi hilo mwaka jana.
The post Hii ndio orodha ya miji 10 yenye mabilionea wengi duniani appeared first on Bongo5.com.