Amnesty International tawi la Nigeria inaripoti kuwa wakulima 43 wa Kijiji cha Maiduguri kilichopo Jimbo la Borno wameuawa na kundi la Boko Haram.

Wakulima 43 wa Jimbo la Borno, Nigeria wamechinjwa katika mashamba ya mpunga, Zabarmari na kikundi cha Boko Haram.

Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ameonesha kusikitishwa na kitendo hicho, pia katika ukurasa wake wa tiwtter ameandika kulaani mauaji hayo.

Serikali ya Nigeria imefanya yote yanayowezekana kulinda nchi hiyo na watu wake, Rais amesema. Aidha shirika la kimataifa linalohusika na haki za binaadamu, Amnesty International lime laani kitend hicho.